Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuzuia mmomonyoko wa barabara ya Dodoma – Iringa katika Mlima wa Nyang’oro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, lakini nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake japokuwa hali ni mbaya sana wakati wa mvua katika lile eneo naomba wajitahidi kufanya haraka sana.

Naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza; kwa kuwa barabara ya Kinyanambo C - Mapanda mpaka Ukami na Kinyanambwa A Saadani – Igoma katika Jimbo la Mufindi Kaskazini ni ya kiuchumi na pia ni ya ahadi ya Mheshimiwa Rais; je, ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami?

Swali la pili, barabara ya Iringa – Kilolo - Idete ni ya mkoa na Serikali iliahidi muda mrefu sana kuiunganisha na mkoa wa Morogoro kupitia kata ya Idete, Itonya, Muhanga mpaka Mungeta; je, ni lini ahadi hiyo itatimia kwa sababu uchumi wa mkoa wa Morogoro na Iringa uweze kukua kwa urahisi zaidi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala hili la barabara ya Kinyanambo C-Mapanda mpaka Ukome. Ni ahadi ya viongozi wetu wa kitaifa na ahadi zote za viongozi wa kitaifa sisi Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tutahakikisha tunazitekeleza na tunaziweka katika vipaumbele vya bajeti ya mwaka 2023/2024, hususani kwenye barabara hii ya Kinyanambo C -Mapanda-Ukoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, barabara hii ya Iringa – Kilolo – Idete kipande cha Ipogolo – Kilolo chenye kilomita 33 ni barabara ambayo inafadhiriwa na Benki ya Dunia na mwaka huu wa fedha tunaoendelea nao, wapo katika hatua za manunuzi na kilometa 67 zilizobaki nazo zimekwishafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa hiyo, niwahakikishie wananchi wa maeneo haya kwa sababu unaunganisha kati ya Mkoa wa Iringa pamoja na Morogoro kwamba inakwenda kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuzuia mmomonyoko wa barabara ya Dodoma – Iringa katika Mlima wa Nyang’oro?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana tulipitisha bajeti hapa ya kujengwa kipande cha Haydom mpaka Labay kwa kiwango cha lami na bajeti ya Waziri bado hatujapitisha.

Je, ni lini atasaini mkataba ule ili barabara ile ijengwe kipande hiki nilichosema kwa kiwango cha lami au tuje na sarakasi kwa namna nyingine tena kwenye bajeti hii ya Jumatatu?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwenye mwaka huu wa fedha tunatakiwa tujenge barabara hii aliyoitamka Mheshimiwa Mbunge na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha kwa sababu mwaka wa fedha wa Serikali ni mpaka tarehe 30 Juni, nina hakika tutakuwa tumesaini barabara hii ili mkandarasi aanze kufanya kazi pale. (Makofi)