Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 339 2023-05-16

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuzuia mmomonyoko wa barabara ya Dodoma – Iringa katika Mlima wa Nyang’oro?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa ujenzi na uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2022/2023, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 250 kwa ajili ya kazi ya kufanya uchunguzi wa miamba na udongo unaomomonyoka katika eneo la Nyang’oro katika Barabara ya Dodoma kwenda Iringa ili kujua tabia za miamba na udongo huo na kuja na mapendekezo ya kitaalam ya jinsi ya kuzuia kumomonyoka huo. Tathmini za zabuni ya kumpata mshauri (consultant) wa kufanya kazi hiyo iko hatua za mwisho na Mkataba utakuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023. Baada ya taarifa ya kitaalam kutolewa, Serikali itatenga fedha za kutekeleza mapendekezo ya kuzuia mmomonyoko huo, ahsante.