Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Barabara ya Mletele - Msamala – Mkuzo hadi Namanditi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM M. NYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika kutokana na ahadi mbalimbali za viongozi wa Serikali, tangu Serikali ya Awamu ya Tatu, yaani mika 23 mpaka sasa uthamini wa maeneo hayo tayari umeshafanyika zaidi ya mara tatu. Sasa naombe nijue;

Je, ni lini wananchi wa maeneo haya watalipwa fidia ili waweze kupisha ujenzi wa barabara hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali jingine, kulingana na uwingi wa malori kulazimika kupita katikati ya mji wa songea hivyo kulazimisha msongamano ajari na uchafuzi wa mazingira.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara ile ili kuweza kupunguza adha inayowakuta wananchi wa Mkoa wa Ruvuma hususani wakazi wa Songea Mjini, kuzingatia kwamba bajeti ya Serikali ya Wizara hii bado haijapitishwa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tathmini tumekwisha kufanya mara tatu, na hii ni kutokana na sheria ya tathmini; kwamba inapofika baada ya miezi sita na kama hakuna malipo yamefanyika inatakiwa tathmini ile iweze kufanyika tena, vinginevyo ilipwe kwa fidia.

Kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi ambao wataathirika katika ujenzi huu ni kwamba tayari sasa tathmini imekamilika, hii ya mwisho, na daftari lipo kwa Mthamini Mkuu wa Serikali ili aweze kusaini na hatimaye Serikali itafute fedha kwa ajili ya kulipa fidia hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kweli tunatambua umuhimu wa barabara hii na ndiyo maana kwa kushirikiana na Benki ya Dunia Serikali imepata mkopo kwa ajili ya ujenzi katika kipande hiki cha Songea - Lutukila na tupo katika hatua za manunuzi.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, mara baada ya manunuzi kukamilika tunaanza kujenga, na iko ndani ya mwaka huu wa fedha.