Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 338 2023-05-16

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga Barabara ya Mletele - Msamala – Mkuzo hadi Namanditi kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Mariam Madalu Nyoka, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ujenzi wa Barabara ya Mletele – Msamala – Mkuzo hadi Namanditi (Songea Bypass) yenye urefu wa kilometa 14 umejumuishwa katika mradi wa ujenzi wa Barabara ya Makambako hadi Songea yenye urefu wa kilometa 280. Sehemu ya kutoka Songea – Rutikira (km 97) ambao unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia chini ya mradi wa Tanzania Transport Integration Project (TanTIP). Maandalizi kwa ajili ya kutangaza zabuni za kumpata mkandarasi wa ujenzi yanaendelea, ahsante.