Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kubadili utaratibu wa malipo kwa wastaafu wa Jeshi la Polisi wa Zanzibar ili kuondoa usumbufu wanaoupata?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali lakini ni ukweli usiopingika kwamba maslahi ya watumishi wa idara hii ya Jeshi la Polisi bado yanahitaji maboresho.

Je, Serikali ina mpango gani mahususi wa kuboresha maslahi ya Askari Polisi ili sasa watakapokuwa wanastaafu waweze kupata mafao ambayo yana endana na hali halisi ya maisha?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashidi Shangazi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa kuangalia maslahi ya askari wa vyombo vya usalama Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameamua kuunda Tume ya Haki Jinai ambayo pamoja na mambo mengine inakwenda kuangalia vilevile eneo hili la maslahi ya askari. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo Mheshimiwa Rais ni katika mambo ambayo anayapa uzito mkubwa sana, na tusubiri pale ripoti ya Tume itakapomaliza ili tione sasa utekelezaji wake utakuwa vipi.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kubadili utaratibu wa malipo kwa wastaafu wa Jeshi la Polisi wa Zanzibar ili kuondoa usumbufu wanaoupata?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kati ya mwezi wa nne mpaka mwezi wa tano kuna mauaji yamefanyika katika Mji wa Sirali wameua mtu pale Kubiterere Mwema wameua mtu katika Kata ya Pemba, wamepiga risasi pale Kiru kwenye kata yangu, na juzi walimuua daktari katika Kituo cha Afya cha Kilende Nyamungo. Kuna kata nane watu wanapigwa risasi hadharani, na hali hiyo haijafuatiliwa. Ningeomba nijue kauli ya Serikali wanachukua hatua gani za dharura ili kurejesha amani katika Jimbo la Tarime na hasa Mji wa Sirali ambao ni mji wa mpakani na biashara kwa kweli imekuwa hali siyo nzuri sana.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waitara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza jambo la kwanza na la muhimu ambalo ningependa Watanzania ambao wanatusikiliza hapa walifahamu ni kwamba hali ya usalama katika nchi yetu ni imara. Matukio ambayo yoyote yanayotokezea katika nchi yetu ya uhalifu wa aina yoyote unaofanywa na mtu yoyote hakuna hata tukio moja ambalo linatokea na polisi ama vyombo vya usalama visifanikiwe kulidhibiti.

Kwa hiyo, mauaji ya aina yoyote ambayo yamekuwa yakitokezea nchini aidha hatua zimeshachukuliwa ama zinaendelea kuchukuliwa. Wako ambao waliohusika wameshapelekwa katika vyombo vya sheria wako ambao uchunguzi unaendelea kufanyika. Na hata suala la jimbo lake, kwa sababu ametoa takwimu, sasa sina hakika kwa aina yake ya kusema ni nani na kwa hiyo siwezi nikamjibu hapa kumwambia tukio hili liko katika hatua gani. Nimhakikishie tu kwamba hakuna sehemu yoyote katika nchi hii ikiwemo katika jimbo la Mheshimiwa Waitara ambapo kutatokea uhalifu wa aina yoyote na vyombo vyetu vya usalama vikiwemo jeshi la polisi vishindwe kuchukua hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, kama ana jambo mahsusi katika jimbo lako ambalo unahisi mpaka sasa hivi hajaridhishwa na hatua iliyochukuliwa naomba, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maswali unipatie taarifa hizo ili tuweze kuzifanyia kazi.