Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya Umwagiliaji ikiwemo kuchimba visima virefu katika Bonde la Dominiki, Kata ya Mwangeza?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri sana ya Serikali yanayotia moyo; hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Halmashauri ya Mkalama inategemea sana vitunguu kwa mapato yake ya ndani.

Je, Serikali haioni haja ya kwamba mpango huu mzuri ufanyike kwa mtindo wa build and design ili uweze kwenda kwa haraka zaidi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa pale Mwangeza kuna mradi wa ASDP two ambao ulibomoka;

Je, Serikali haioni sasa haja ya kuukarabati mradi huo haraka ili wananchi wa pale mwangeza waendelee kupata umwagiliaji wakati wakisubiri hili bonde la vitunguu kufanyiwa design?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika miradi yote ya umwagiliaji ambayo tumeipita nchi nzima utaratibu unaofanyika hivi sasa ni kuhakikisha kwanza tunaanza na upembuzi yakinifu na baadaye ndipo unakuja usanifu wa kina na kisha twende kwenye ujenzi. Hii ni kwa sababu tulipata changamoto ya miradi mingi sana ya miaka iliyopita ambayo haikupitia hatua hii na hivyo imekuwa ikibomoka kwa haraka sana. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba miradi hii inakuwa endelevu na ya kudumu ili wakulima waweze kunufaika. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge wavumilie taratibu hizi zikamilike mradi huu utajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili la kuhusu Mwangeza. Katika kiambatisho cha saba katika jedwali lile la bajeti yetu eneo la Mwangeza ni kati ya maeneo ambayo yanakwenda kufanyiwa upembuzi yakinifu na baadaye pia tutajenga skimu na kukarabati ili wakulima waweze kupata fursa ya kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji. Kwa hiyo ni eneo ambalo lipo ndani katika mipango ya Serikali tayari.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya Umwagiliaji ikiwemo kuchimba visima virefu katika Bonde la Dominiki, Kata ya Mwangeza?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Jimbo la Kalenga lina skimu 19 za umwagiliaji ambazo miundombinu yake yote ni chakavu.

Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba miundombinu hii inaboreshwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 tumetenga maeneo zaidi ya 80 ambayo yanakwenda kufanyiwa ukarabati zikiwemo skimu zilizo katika Jimbo la Kalenga. Kwa hiyo nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, anaweza kupitia akaangalia orodha yetu na akaona kama maeneo yao yapona aweze kujiridhisha.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya Umwagiliaji ikiwemo kuchimba visima virefu katika Bonde la Dominiki, Kata ya Mwangeza?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii; je, ni lini Serikali itajenga bwawa na mifeji kwa ajili ya umwagiliaji katika Kata za Shambalaiguruka na Majengo kwa lengo la kupunguza athari za mvua na mafuriko ya Mto Nduruma na Mto Chiplepa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti yetu inayokuja tumetangaza kwamba tunaenda kujenga mabwawa 100 ambayo yatagusa takriban maeneo yote nchi nzima. Hivyo katika wilaya ya kwake Mheshimiwa Mbunge tunakwenda kuangalia maeneo ambayo amaeyataja. Kama si hayo basi tutaichukua kama sehemu pia ya kuifanyia kazi ili katika wakati mwingine ujaotuweze kuyajenga pia.