Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 336 2023-05-16

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya Umwagiliaji ikiwemo kuchimba visima virefu katika Bonde la Dominiki, Kata ya Mwangeza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Bonde la Dominiki lipo katika Kata ya Mwangeza Halmashauri ya Mkalama. Bonde hili ni kati ya maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji yaliyobainishwa na kutambuliwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ndani ya Halmashauri ya Mkalama. Bonde la Dominiki lina takribani hekta 800 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Hata hivyo kwa sasa wakulima wa bonde hili hutegemea kilimo cha mvua. Hii ni kutokana na kutokuwa na uwekezaji wa aina yoyote ya miundo mbinu ya umwagiliaji na chanzo cha kudumu cha maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mpango na bajeti ya mwaka 2023/2024 imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kupata gharama halisi za kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji katika Bonde hilo.