Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaachia bei ya zao la kahawa kuamuliwa kwa nguvu ya soko?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru nina maswali mawili ya nyongeza. Ningependa kupata kauli ya Serikali, kule kwetu Muleba wakulima wanafukuzwa wanakamatwa wakisafirisha kahawa kutoka kata moja hadi kata nyingine na katika tarafa hadi tarafa nini kauli ya Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; nilitaka kujua kahawa ni mali ya nani? Ni mali ya Serikali au ni mali ya mkulima? Na ni lini ile hadhi inabadilika? Nashukuru sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge Dkt. Kikoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, kauli ya Serikali ni marufuku kwa wakulima wa kahawa walioko katika eneo moja kukamatwa na kuzuiwa kufanya biashara yao kwa sababu biashara hii inafanyika kwa mujibu wa Sheria Na. 23 ya mwaka 2001.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, zao la kahawa kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge, katika hali yake ya kawaida Serikali inafanya uratibu lakini mazao haya ni ya wakulima. Najua alikuwa anaelekea wapi, lakini lengo kubwa la Serikali ni kuhakikisha kwamba tunasimamia na kumfanya mkulima wa kahawa aweze kunufaika. Kwa hiyo kama Serikali tutaendelea kuhakikisha kwamba tunaweka mazingira wezeshi ili mkulima wa kahawa aweze kunufaika.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaachia bei ya zao la kahawa kuamuliwa kwa nguvu ya soko?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mnada wa Kahawa wa Songwe ni tofauti kabisa na mnada wa kahawa uliopo kule Kagera. Mazingira ya pale Songwe siyo rafiki, hauko wazi na kuna uhuni mwingi unaofanywa na baadhi ya wanunuzi kwa kushirikiana na watu wa bodi kuchezesha bei ya kahawa kwenye mnada ili wakulima wasipate bei inayostahili.

Je, kwa nini Serikali isiboreshe mazingira ya mnada wa kahawa wa Songwe ufanane kama mnada wa kahawa wa Kagera ambao uko wazi fair na hakuna uhuni wowote unaoweza kufanyika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge George Mwenisongole, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kagera inalimwa robusta, Songwe inalimwa arabica. Haya ni variety mbili tofauti. Ukienda kwenye soko ili uweze kuuza kahawa ya arabica lazima pia ionjwe ndio unapata radha na quality inayokwenda ku-determine bei. Tumesikia hoja ya Mheshimiwa Mbunge naelekeza bodo ya kahawa kuhakikisha kwamba wanaweka mazingira wezeshi ili pia mkulima wa Songwe aweze kunufaika na bei ya kahawa.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaachia bei ya zao la kahawa kuamuliwa kwa nguvu ya soko?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT M. BILAKATWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Zao la kahawa limevamiwa na ugonjwa wa mnyauko.

Je, Serikali iko tayari kuongeza miche yenye ubora ili zao hili muhimu lisije likafutika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa; na katika bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 tumeongeza miche kufikia miche milioni 20 ili wakulima waweze kupata miche bora ambayo pia itakuwa na ukinzani wa magonjwa ambayo yanaathiri zao la kahawa.