Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 335 2023-05-16

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaachia bei ya zao la kahawa kuamuliwa kwa nguvu ya soko?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bei ya kahawa duniani hutegemea mwenendo wa bei katika masoko ya rejea ya kahawa duniani ambayo ni soko la bidhaa la New York (ICE) kwa kahawa za arabika na euronest LIFFE ya London kwa kahawa aina ya robusta. Mabadiliko ya mwenendo wa bei katika masoko hayo huchochewa na kiasi cha kahawa kilichozalishwa duniani na mahitaji kwa wakati husika.

Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya mwenendo wa bei ya kahawa katika masoko rejea yana athari za moja kwa moja kwenye bei za kahawa katika masoko ya kahawa hapa nchini na duniani kwa ujumla. Hivyo, Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi yanayoleta ushindani wa kutosha ili kuchochea bei ya kahawa nchini.