Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasimika taa kwenye barabara za mitaa Mji wa Masasi ili kuongeza usalama, kupunguza uhalifu na kuhamasisha shughuli za biashara?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nina maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyatoa ningependa kujua kwamba Serikali inafikiriaje kwa halmashauri ambazo hazina uwezo mkubwa kimapato wa kuweza kugharamia uwekaji wa taa barabarani kupitia ruzuku inayotolewa na REA kwamba halmashauri hiyo ikapata ruzuku asilimia 75 mpaka 100 ukilinganisha na asilimia 50 ya sasa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni kwamba, sasa hivi tunajua tunafanya juhudi kubwa ya kujenga barabara za mijini hususani pale Masasi na kwenye majimbo ya wenzangu. Kwa nini TAMISEMI sasa isiamue kufungamanisha fedha ambazo zinatolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara na fedha kwa ajili ya uwekaji wa taa ili Mkandarasi anayepewa kujenga zile barabara pale mjini anamalizia na kuweka taa moja kwa moja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwambe, la kwanza hizi Halmashauri ambazo haazina uwezo kupata ruzuku ya REA. Hili tunalichukua kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI na tutahakikisha tunakaa taasisi yetu ya TARURA kwa kushirikiana na taasisi ya REA ambayo iko chini ya Wizara ya Nishati kuona ni namna gani tunaweza kufanya kazi ka Pamoja na kutoa hiyo ruzuku iende kwenye barabara hizi kwenye miji ambayo haina uwezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, kwa sasa barabara zote zinazojengwa na TARURA nchini kote hasa zile zinazopita kwenye Katikati ya miji zinawekewa taa. Pia, kama Masasi kule hawajaanza naamini wakimaliza tu katika ujenzi wa barabara hizi taa zitaanza kufungwa kama nilivyokuwa nimesema kwenye majibu yangu ya msingi.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasimika taa kwenye barabara za mitaa Mji wa Masasi ili kuongeza usalama, kupunguza uhalifu na kuhamasisha shughuli za biashara?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mji wa Mugumu kama unakuwa kwa kasi na shuguli za maendeleo wakati wote zinaendelea.

Je, ni lini sasa Serikali itatusaidia kuhakikisha tunapata taa za barabarani katika mji wa Mugumu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejipanga kuweka taa katika mji wa Mugumu kwenye barabara zinazokamilika. Mheshimiwa Mbunge ni shahidi kuna barabara inayozunguka Soko kuu la Mugumu ambayo inakamilika muda si mrefu na barabara ile itakapokamilika taa zile zitafungwa kama nilivyosema awali kwamba sasa TARURA katika barabara zote zinazojengwa katikati ya miji ni lazima ziwekewe taa.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasimika taa kwenye barabara za mitaa Mji wa Masasi ili kuongeza usalama, kupunguza uhalifu na kuhamasisha shughuli za biashara?

Supplementary Question 3

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri, alipokuja Katibu Mkuu wa CCM, Kiteto alituahidi taa za barabarani pale mji wa Kibaha na tumeleta maombi. Ni lini Serikali itatuletea hizi fedha tuweke taa za barabarani pale mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema ilikuwa ni ahadi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ambae Serikali hii ndio inatekeleza Ilani yake ya uchaguzi, tutakaa na wenzetu wa TARURA ambao ni taasisi iko chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuona wamejipangaje katika kutekeleza uwekaji wa taa hizi kama ambavyo Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi inavyotaka.