Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 334 2023-05-16

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasimika taa kwenye barabara za mitaa Mji wa Masasi ili kuongeza usalama, kupunguza uhalifu na kuhamasisha shughuli za biashara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Masasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwepo kwa uhitaji wa taa za barabarani katika Halmashauri ya Mji wa Masasi kutokana na kukua kwa shughuli za kimaendeleo, kiuchumi na kijamii.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa wedha wa 2022/2023, Serikali kupitia TARURA - Wilaya ya Masasi imetenga shilingi milioni 192 kwa ajili ya kusimika taa 48 kwenye barabara za Mji wa Masasi ambazo zitawekwa kwenye barabara za TANESCO - Yatima na Barabara ya Mkapa.