Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, mashine ngapi za kukusanya mapato zilibainika kutokuwa hewani na hazikutambulika na Halmashauri mwaka 2018/2019, 2019/2020 na 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH. J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa maboresho yaliyofanywa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Kwa kuwa changamoto kubwa ya mkaguzi wa nje CAG katika POS ilikuwa ni matumizi ya fedha mbichi na kusababisha kushuka kwa mapato ya hamashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kufahamu je, mfumo mpya wa TAUSI unakwenda kukabiliana nayo vipi hii changamoto?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakusanya mapato wengi hawana taaluma. Nilitaka kujua mkakati wa Serikali wa kuajiri wahasibu wa kutosha katika halmashauri zetu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la kwanza nianze kwa kusema changamoto kubwa ambayo ilikuwepo kwenye halmashauri zetu na hizi POS kuwa ziko offline ilikuwa ni uadilifu wa watumishi wetu. Tayari Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilichukulia hatua wale wote waliopatikana na hatia ya kucheza na POS hizi na hivyo kupotezea mapato halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna Dashboard hivi sasa katika mfumo mpya wa TAUSI ambapo katika halmashauri zote, Mkurugenzi ana uwezo wa kuona mapato yaliyokusanywa kwa wakati huo na kama kuna POS yoyote itakwenda offline basi nayo Mkurugenzi ataona. Hata hiyo, dashboard ile ile iko Mkoani na vilevile Ofisi ya Rais, TAMISEMI tuna uwezo wa kuona. Kwa hiyo, tumefanya maboresho makubwa sana na kuanzia tarehe 1 Julai ndio mfumo pekee ambao utatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali la pili; la taaluma, Kuajiri watu wenye taaluma ya uhasibu. Hili tunalipokea na kadri ya uwezo wa Serikali wa kibajeti tutaajiri watu kuendana na taaluma ya uhasibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, mashine ngapi za kukusanya mapato zilibainika kutokuwa hewani na hazikutambulika na Halmashauri mwaka 2018/2019, 2019/2020 na 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa hii nafasi. Kwa kuwa Serikali imekuja na mfumo mpya wa kukusanya mapato unaojulikana kama TAUSI, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba madiwani wote wanapata elimu ya huu mfumo? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali kwenye mfumo huu wa TAUSI, kwanza ni Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilitoa technical specification kwa halmashauri zote za aina ya POS ambazo zinatakiwa kununuliwa ambazo zitaendana na mfumo huu. Kadri tunavyokwenda tunatoa mafunzo kwa wale wanaohusika na POS hizi kule kujua ni namna gani wanatumia POS hizi ambazo zinaendana na mfumo huu wa TAUSI.