Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 333 2023-05-16

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, mashine ngapi za kukusanya mapato zilibainika kutokuwa hewani na hazikutambulika na Halmashauri mwaka 2018/2019, 2019/2020 na 2020/2021?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 kulikuwa na mashine 14 za kukusanyia mapato (POS) katika halmashauri mbili, mwaka 2019/2020 kulikuwa na mashine 1,469 za kukusanyia mapato (POS) katika halmashauri 54 na mwaka 2020/2021 kulikuwa na mashine 1,355 katika halmashauri 46 ambazo hazikuwa hewani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imefanya maboresho ambapo matumizi ya mashine za kukusanyia mapato kupitia mfumo wa LGRCIS yatakoma ifikapo tarehe 30Juni, 2023 hivyo kuanzia tarehe 1 Julai, 2023 hakutakuwa na POS zitakazokuwa offline zaidi ya saa 24.