Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika Kata ya Mletele Wilayani Songea?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri sana ya Serikali, pamoja na hivyo bado naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Sera ya Taifa inaeleza kwamba maeneo ya pembezoni mwa Miji na Manispaa yatakwenda kuwekewa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 na siyo shilingi 300,000 kama ilivyo sasa.

Je, ni kwanini Serikali inakwenda kinyume na sera yake yenyewe? (Makofi)

Swali la pili, je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata zenye mazingira ya vijijini ambazo ni Rilambo, Shibira, Dilimalitembo, Mletele, Shule ya Tanga, Mwengemshindo, Mbati na Wenje? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza la kuhusu bei ya shilingi 27,000 kwenye sera, naomba kuliarifu Bunge lako kwamba bei zinazotumika kuunganisha umeme kwa wateja wa TANESCO zinapangwa na kusimamiwa na Mamalaka ya Udhibiti ya EWURA. Kwa hiyo, kinachofanywa ni kuangalia maeneo maalum na kuyapangia bei yake. Maeneo ya vijijini ni shilingi 27,000 maeneo ya mijini ni shilingi 321,000 na kuendelea.

Mheshimiwa Spika, ilijaribiwa kufanyiwa shilingi 27,000 kila sehemu lakini kwa uhalisia ilionekana ni ngumu, lakini zoezi la kuendelea kubaini ni kiasi gani kitumike kuunganisha eneo gani kinaendelea kama ambavyo tumekuwa tukitoa taarifa na jambo hilo litakapokamilika basi bei nzuri za kila eneo zitatangazwa ili ziweze kutumika.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili. Kuhusu umeme kupelekwa katika maeneo ya vijijini lakini yaliyoko mijini tunafanya hivyo, kwenye baadhi ya maeneo tayari kuna awamu ya kwanza ilishafanyika kwa Mikoa kadhaa, awamu ya pili imefanyika na sasa inaendelea awamu ya tatu. Nimhakikishie Mheshimiwa Msongozi kwamba katika maeneo aliyoyataja nayo yamo katika plan za Serikali na upatikanaji wa fedha utakavyokuwa tayari maeneo hayo pia yatapelekewa umeme katika maeneo ya mijini yenye uso wa vijijini kwa kadri ya upatikanaji wa fedha katika siku chache zijazo. Nashukuru.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika Kata ya Mletele Wilayani Songea?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kutokana na tatizo kubwa la umeme tulilonalo Wilayani Urambo, ni lini kituo kinachojengwa Kata ya Vumilia eneo la Uhuru litakamilika kama utatuzi wa tatizo hilo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Kituo cha Uhuru kilichopo Urambo ni mojawapo ya vituo 14 vinavyojengwa katika mradi wetu wa Gridi Imara na kabala ya mwaka huu kuisha kituo hicho kitakuwa kimekamilika kwa sababu tayari mashineumba (transformer) zimeshakaguliwa kiwandani na sasa zimefungwa kwa ajili ya kuja kuwekwa katika kiwanda hicho kwa sababu jengo tayari lilishakamilika na lane inaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Spika, hivyo, kabla ya mwaka huu kuisha kitakuwa kimekamilika ili kuweza kuhudumia wananchi. (Makofi)

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika Kata ya Mletele Wilayani Songea?

Supplementary Question 3

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mkoa wa Kigoma unaunganishwa katika Gridi ya Taifa, mpaka sasa Wilaya za Kigoma na Uvinza bado hazijaunganishwa. Je, ni lini Serikali itakamilisha kazi ya kuunganisha Wilaya hizi ili kukamilisha Mkoa wa Kigoma? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kigoma umeunganishwa kwa Gridi ya Taifa kwa line ndogo inayotoka katika kituo chetu cha kupoza Umeme cha Nyakanazi na line hiyo ya msongo wa kilovolti 33 iliishia maeneo ya Kibondo, lakini tayari mradi mkubwa wa kilovolti 400 unaojengwa kutoka Nyakanazi kwenda Kidahwe Mjini Kigoma wa kilometa 280 unaendelea, kabla ya mwaka 2025 utakuwa umekamilika na hivyo Mkoa wote wa Kigoma utapata huduma ya umeme wa Gridi ya Taifa.