Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 299 2023-05-11

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika Kata ya Mletele Wilayani Songea?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mletele katika Manispaa ya Songea ina jumla ya mitaa sita ambayo ni Mletele, Makemba, Liumbu, Nonganonga, Mdundiko na Mji Mwema. Mitaa mitano ya Mletele, Makemba, Liumbu, Nonganonga na Mdundiko tayari ina umeme. Mtaa wa Mji Mwema tu ndiyo bado haujafikiwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, mtaa huu tayari umefanyiwa tathmini na utapata umeme kwa kuweka miundombinu itakayogharimu shilingi 115,767,782.60 katika Mwaka wa Fedha 2023/2024. Nashukuru.