Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka wapimaji wa miamba ya madini katika Mikoa ya Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza kabisa nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini pamoja na hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali tayari ina taarifa za miamba yenye madini katika Mkoa wa Rukwa na Songwe. Je, ni lini sasa itatoa taarifa na kusambaza kwa wananchi ili wananchi hawa waweze kuomba leseni kwa ajili ya uchimbaji? (Makofi)

Swali la pili, ni nini sasa mpango wa Serikali kwa kuwapa mitaji wachimbaji wadogo wakiwemo wanawake? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, taarifa za kijiolojia za maeneo yenye madini nchini hutolewa na GST kupitia chapisho la kitabu cha madini yapatikanayo Tanzania ambacho toleo la mwisho lilitolewa mwaka 2019. Kutokana na tafiti zilizoendelea kuna aina nyingi za madini zimeendelea kugundulika na hivyo toleo la tano limekamilika, tuko kwenye hatua za kuandaa uzinduzi wa kitabu kipya cha madini hayo na siku ya uzinduzi wa hicho kitabu tutawaalika Wabunge wote na wadau mbalimbali wa madini waweze kupata nakala ya vitabu hivyo ili taarifa hizi ziweze kuwafikia walengwa katika maeneo ya Wilaya zote za nchi yetu.

Swali lake la pili kuhusu mpango wa kuwapatia wachimbaji wadogo mitaji ulikwishawekwa kupitia maelewano na mabenki ya ndani, kwamba watoe mikopo kwa wachimbaji wadogo waliokidhi vigezo na tayari mabenki ya ndani yameshatoa zaidi ya shilingi bilioni 145 kwa wachimbaji wadogo wenye leseni, ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka wapimaji wa miamba ya madini katika Mikoa ya Rukwa na Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Wilaya ya Nyang’hwale wachimbaji wadogo wadogo wameendelea kuvumbua maeneo mbalimbali kama vile Isonda, Igalula, Isekeli, Shibalanga, Ifugandi, Rubando, Lihulu, Bululu pamoja na Mahagi.

Je, Wizara ina mpango gani wa kupeleka mitambo ya kufanya utafiti ili uchimbaji ule uwe wa kuendelea?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa upande wa kupeleka mitambo ya kuwasaidia wachimbaji wadogo, Wizara kupitia taasisi yake ya STAMICO imeagiza mitambo mitano ambayo tayari ilishaagizwa na mingine mitano pia imeshaagizwa kwa ajili ya kuwa na zana mahsusi kwa ajili ya kusaidia uchimbaji wa wachimbaji wadogo waweze kufanyiwa upimaji wa maeneo yao wajue aina ya madini na kiasi kinachopatikana.