Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Madini 298 2023-05-11

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka wapimaji wa miamba ya madini katika Mikoa ya Rukwa na Songwe?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imekwishafanya utafiti wa miamba katika Mikoa ya Rukwa na Songwe na kuchora ramani za miamba katika kipimo cha skeli ya 1:100,000 ambazo hutumika kuonesha uhusiano wa miamba na madini. Ramani hizi za miamba zinapatikana GST na ndizo kwa sasa hutumika kuvutia uwekezaji katika sekta ya madini kwa maeneo hayo. Ahsante sana.