Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kufufua Kiwanda cha Maziwa Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na majibu ambayo ni mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, tatizo la kiwanda siyo tu wanahisa, tatizo la kiwanda ni deni la Benki yetu ya Kilimo.

Swali la kwanza, je, Waziri haoni haja sasa ya kuhakikisha kwamba anaratibu majadiliano akishirikisha Wizara ya Mifugo ambayo ndiyo inasimamia sekta hiyo kwa haraka sana? (Makofi)

Swali la pili, anawahakikishiaje Wananjombe na wafugaji wa Njombe kwamba majadiliano hayo sasa yatafanyika kwa haraka katika kipindi hiki cha Bunge au mara tu baada ya kuisha Bunge hili? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kama nilivyosema nia ya Serikali ni kuona kiwanda hiki kinafanya kazi na kwa taarifa tu kwa sababu ya umuhimu wake Wizara wenye dhamana ya kuhakikisha maendeleo ya viwanda nchini yanafanikiwa na kuwa na tija, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaratibu majadiliano ya wanahisa kwa maana ya NJOLIFA, Njombe Wilaya, Njombe Mji, Roman Catholic ambao nao wanahisa na wengine. Muhimu zaidi kama nilivyosema moja ya sababu iliyopelekea kukwama kiwanda hiki ni mtaji ambao sasa kupitia Benki ya Kilimo (TADB) ilitoa zaidi ya shilingi bilioni 1.6. Sasa tutaandaa kikao, tutawaita kabla ya kuisha Bunge hili ili wanahisa wote na wenzetu wa TADB tuje tukae hapa, tuone namna gani tunakwamua mkwamo wa kiwanda hiki ili kiendelee kuzalisha kwa tija lakini pia kupata manufaa kwa nchi katika sekta ya viwanda.