Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 297 2023-05-11

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kufufua Kiwanda cha Maziwa Njombe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto za kiwanda cha maziwa Njombe Milk Factory Company Limited na Serikali kupitia uongozi wa mkoa imekwishaanza kuchukua hatua za kukikwamua kiwanda hicho. Hatua za awali zilizochukuliwa ni pamoja na kuwakutanisha wanahisa wa kiwanda na uongozi wa Mkoa wa Njombe.

Aidha, ninapenda kumuahidi Mheshimiwa Mbunge kuwa, kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Njombe, Serikali itahakikisha kiwanda hicho kinaweza kufufuliwa kwa haraka ili sekta ya viwanda vya maziwa izidi kukua na kuleta manufaa kwa wafugaji na wanahisa, ninakushukuru.