Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Kilambo?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini swali la kwanza; ni lini upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utafanyika kwenye daraja hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali ya Mozambique iko tayari kutoa ushirikiano wa ujenzi wa daraja hilo, ni lini mazungumzo haya yatakuwa yanaendelea kwa kina? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kutambua umuhimu wa barabara hii kwa upande wa Tanzania, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi upande wa Tanzania tuko tayari kuijenga hiyo barabara na katika mwaka huu wa fedha ambao tunakwenda kuleta bajeti, tumeweka fedha kwa ajili ya kuanza kufanya maandalizi ya kufanya usanifu na kufanya upembuzi na usanifu wa kina, lakini kama nilivyosema kazi hiyo itaanza tu pale ambapo tutakuwa tumekamilisha na wenzetu wa Msumbiji kwa sababu ni daraja la pamoja, ahsante. (Makofi)