Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mzumbe hadi Mgeta?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ni lini barabara ya Gairo hadi Milima ya Nongwe ambayo ni agizo la viongozi wa kitaifa, itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; barabara ya Ifakara – Mbingu – Chika – Mlimba ni mbovu sana; je, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Gairo kwenda Nongwe ni barabara ya mkoa ambayo haijafanyiwa upembuzi yakinifu wala usanifu wa kina. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii TANROADS kupitia Mkoa wa Morogoro wameomba iwekwe kwenye upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa maana ya kufanya maandalizi ya kujenga kwa kiwango cha lami kwa mwaka huu wa fedha tunaouendea.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara aliyoitaja ya Ifakara - Mlimba - Kibena. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita tayari ilishatangaza barabara hii kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ambapo imegawanya katika lot mbili kuanzia Ifakara hadi Mbingu na Mbingu hadi Chita. Kwa hiyo, tayari iko kwenye hatua za manunuzi na tunategemea kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha barabara hii itakuwa pengine imeshaanza kujengwa, ahsante.