Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 294 2023-05-11

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mzumbe hadi Mgeta?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Mzumbe kuanzia Eneo la Sangasanga – Langali – Luale hadi Kikeo, yenye urefu wa kilometa 59.16 ambapo jumla ya kilometa 13.5 za lami zimejengwa na zimekamilika kwenye maeneo korofi yenye maporomoko na milima mikali. Aidha, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara hii kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.