Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Afya katika Kata ya Segera, Tarafa ya Mkumbulu kitajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini kule kwenye Tarafa ya Kwamsisi ni tarafa iliyoko pembezoni sana. Sasa ni lini Serikali itaona umuhimu wa kujenga Kituo cha Afya katika Kata ya Kwa Msisi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Handeni Vijijini tuna upungufu mkubwa sana wa watumishi, takribani tuna upungufu wa zaidi ya asilimia 60. Sasa je, ni mkakati gani wa Serikali katika kupambana na upungufu huo wa watumishi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA YA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la kwanza la Tarafa ya Kwamsisi ni lini itapata kituo cha afya; nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mwaka wa fedha 2024/2025, tarafa hii na Kata ya Kwa Msisi itatengewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya.

Mheshimiwa Spika, nikienda katika swali lake la pili la upungufu wa watumishi, kama ambavyo wote ni mashahidi katika Bunge lako hili tukufu, Serikali inaendelea kuajiri na hivi sasa kuna ajira zaidi ya 21,000 ambazo zimetangazwa na Serikali itaendelea kuajiri vile vile kadri ya uwezo wake wa kibajeti na katika hawa watumishi 21,000 ambao wanaajiriwa hivi karibuni vile vile Handeni Vijijini watapata watumishi.