Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FROLENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza minara au kuboresha mawasiliano katika kata zote 20 za Wilaya ya Misenyi?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali na niipongeze baada ya kipindi cha miaka miwili baada ya ziara ya Naibu Waziri, katika jimbo langu tumekwishapata minara Minne mipya. Pia, nashukuru katika bajeti mpya sasa hiyo minara mipya minne ikienda kujengwa tutaielekeza katika maeneo yanayohusika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Misenyi, kama ilivyo mpakani mwa Nchi ya Uganda imekuwa na changamoto kubwa ya mawasiliano. Sasa ni lini minara mingine itajengwa katika Kata za Bugandika, Kilimilile, Buyango, Kitobo, Bwanjai na Mabale ili kuweza kufanya wananchi wa maeno hayo waweze kupata mawasiliano mazuri katika jimbo letu?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, wananchi wa Wilaya ya Misenyi, wamekuwa wakipata mawimbi ya redio ya nchi jirani ya Uganda. Ni lini sasa Serikali itaweka nia ya dhati kuhakikiasha kwamba wananchi wanafaidi mawasiliano ya mawimbi ya radio ya nchi yetu? Ahsante sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kyombo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunafanya feasibility study kwa ajili ya kupeleka huduma ya mawasiliano katika Kata ya Bugorora na Kakunyu hapakuwa na minara imejengwa. Lakini kwa sasa tumegundua watoa huduma kwa kutumia uwekezaji wao wamekwisha jenga minara katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa minara ambayo tulikuwa tumepanga kupeleka pale sasa tutaihamishia na kupeleka Kata ya Minzilo na tutapeleka katika eneo la Kashenye. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, wananchi wa eneo hilo pamoja na maeneo ya Kitobo na Kanyigo wote tutawaweka katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipengele cha pili, eneo la Misenyi lina changamoto ya huduma ya usikivu wa redio. Pia, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari ametoa fedha kwa ajili ya kwenda kujenga kituo katika eneo la Kyerwa ambapo tukishafunga mtambo wetu pale utaweza kufikisha huduma ya redio katika maeneo ya Misenyi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. FROLENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza minara au kuboresha mawasiliano katika kata zote 20 za Wilaya ya Misenyi?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Katika bajeti hii tunayomalizia ya 2022/2023 Serikali ilikuwa imepanga kujenga minara ya mawasiliano katika Kata za Urushimbwe, Mabogini na Kibosho Kati. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusiana na ujenzi wa minara hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Profesa Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kulikuwa na changamoto hii na Mheshimiwa Mbunge, aliwasilisha changamoto hii mara kwa mara lakini Serikali ilijitahidi sana kutafuta fedha na hatimae Mheshimiwa Rais, ametoa fedha na tunakwenda kuingia mkataba na kampuni ya Vodacom na TIGO kwa ajili ya Urushimbwe, Mabogini pamoja na eneo la Kibosho kati. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge hili tuna uhakika kwamba kati ya Mwezi wa Sita au wa Saba tayari ujenzi wa mnara huo utaanza rasmi.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. FROLENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza minara au kuboresha mawasiliano katika kata zote 20 za Wilaya ya Misenyi?

Supplementary Question 3

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga minara katika Kata ya Shigala, Nyaruhande na Kijiji cha Kijereshi ili kuboresha mawasiliano kwa sababu kata hizi zinashida kubwa ya mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa niwajulishe watanzania, Waheshimiwa Wabunge, tarehe 13 Mei, 2023 tunakwenda kusaini Mkataba wa kufikisha huduma ya mawasiliano katika kata 713 ambayo ni wilaya 127 mikoa yote, ambapo ni Vijiji takribani 1407. Watanzania takribani milioni 8.5 wanakwenda kupata huduma ya mawasiliano, ambapo Mheshimiwa Rais, ameidhinisha kiasi cha bilioni 125.9 kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano katika maeno hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nitumie Bunge lako Tukufu kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wahudhurie katika hafla ya utiaji Saini wa mikataba hii ambayo inakwenda kufikisha huduma ya mawasiliano kote Tanzania.