Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwanza napenda kuishukuru sana Serikali kwa ujenzi wa hii barabara kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza. Kwa kuwa Serikali imewekeza ujenzi wa bandari pale Karema, ujenzi ambao ni mkubwa sana: Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba barabara ya kutoka Kagwila kwenda Karema inafanyiwa ukarabati, kwani kwa sasa hivi imeharibika sana?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kumekuwa na matatizo watu wanapopisha ujenzi wa barabara, Serikali imekuwa na tabia ya kuchelewesha kuwalipa: Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi watakaopisha ujenzi wa barabara inayojengwa kwa kiwango cha lami toka Kagwila kwenda Karema?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nipokee shukurani kwa niaba ya Mheshimiwa Rais, kwa sababu shukurani hizo ni zake, ndiye anayetoa hizo fedha kujenga hiyo miundombinu. Kwa maswali yake mawili, nakubali kwamba barabara ya Kagwila kwenda Karema kilomita 112 inayoenda kwenye Bandari ya Karema ilikuwa na changamoto, lakini Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba Mkoa kupitia Meneja, waliomba fedha za ziadam Shilingi milioni 500 tulishatoa, na wako wanakarabati maeneo yale ambayo yalikuwa hayawezi kupitika hasa maeneo ambayo wanalima mpunga karibu na barabara. Kwa hiyo, kwa sasa tunavyoongea, Mheshimiwa Mbunge barabara ile inapitika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu fidia, tayari tumeshakamilisha tathmini na wananchi wote ambao watalipwa kwa mujibu wa sheria zetu kwa barabara ya Kagwila hadi Karema, tayari wameshatambuliwa na tayari wameshajulishwa kila mtu atalipwa kiasi gani. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itawalipa wote watakaopisha barabara kwa mujibu wa sheria, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Barabara ya Nangulukulu - Liwale, inayopita katika majimbo ya Kilwa Kusini, Kilwa Kaskazini na Liwale, imeharibika vibaya kutokana na mvua za hivi karibuni. Nini maelekezo ya Wizara, kuelekeza TANROADS Mkoa wa Lindi kufanya marekebisho katika maeneo ya Nangulukulu - Migelegele – Mbate, Naiwanga – Njinjo – Miguluwe mpaka Kimambe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii kama tulivyosema huko nyuma na tulikwishatoa maelekezo na ninatoa sasa maelekezo mahususi kwa Meneja wa Mkoa wa Lindi, kuhakikisha kwamba anakwenda maeneo yote ya barabara ya Nangulukulu – Liwale kurekebisha maeneo yote ambayo hayapitiki kwa sasa na kama kutakauwa na changamoto ya kibajeti basi aweze kuwasiliana na TANROADS Makao Mkauu kwa msaada zaidi ili kuhakikisha kwamba anarejesha mawailiano.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Barabara ya Singida kupitia kwamtoro mpaka Kedashi - Tanga, ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu na kwa sababu mlituambia tayari imekwishawekwa kwenye mpango wa kujengwa, na imetangazwa katika kilomita 2100. Ni lini sasa mkandarasi atakuja kwa ajili ya kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba barabara hiyo tuna mpango thabiti wa kuijenga kwa kiwango cha lami. Kama tulivyokuwa tunaelezea kwamba nitajengwa kwa mpango wa EPC+F na ninaomba Mheshimiwa Mbunge, avute subira ataisikia tutakapokuwa tunawasilisha bajeti yetu. (Makofi)