Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, kwa nini ilitumika njia ya single source kumpata Mkandarasi wa SGR Lot No. 6 Tabora – Kigoma na kusababisha hasara ya trilioni mbili?

Supplementary Question 1

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Moja, kwa nini Wizara na TRC waliacha bei ya ushindani ya shilingi bilioni 9.1 kwa kilometa moja ya standard gauge na kuamua kumpa kampuni ya CCECC kwa shilingi bilioni 12.5 kwa kilomita moja ya standard gauge na kuisababishia hasara Serikali ya shilingi trilioni mbili ambayo ni kinyume na matakwa ya single source kama alivyoeleza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ni kwa nini Serikali isivunje huo mkataba baina ya TRC na CCECC wa ujenzi wa kipande cha Tabora - Kigoma kwa sababu hata hiyo Lot III, Lot IV anayoi-refer CAG ameshatuambia kwamba tayari walikiuka utaratibu wa sheria. Kwa nini Serikali isifute huu mkataba wa kinyonyaji?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu bei ya ushindani, bei zilizopo ni tofauti sana na zilizotumika miaka ya 2017 wakati nchi inaanza ujenzi wa standard gauge. Kila kitu kimebadilika, hususan katika suala la asilimia zaidi ya 65 ya SGR, inatumia chuma. Bei ya Soko la Dunia ya chuma, imeongezeka kwa robo tatu ya gharama yake. Pia mwaka 2017 bei ya mafuta ilikuwa takribani shilingi 1,900, sasa hivi imekwenda mpaka shilingi 3,000 na kitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo gharama anazolinganisha Mheshimiwa Mpina, ziko tofauti sana na gharama za leo. Hata hivyo, hapa tumesema katika jibu letu la msingi kwamba tumeokoa takribani shilingi bilioni 632.74. Katika nchi za Afrika Mashariki, sisi Tanzania peke yake, kwa gharama ya ushindani, ndiyo tumeweza kuwa na kiwango kidogo zaidi cha kutengeza kilomita moja kwa dola za Kimarekani milioni nne, wakati nchi jirani na hata ukisoma ripoti ya Benki ya Dunia, ni zaidi ya dola za Kimarekani kwa kilomita moja milioni 7.69. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nihakikishie Watanzania na Bunge lako tukufu kwamba hakuna hasara yoyote, zaidi tumeokoa fedha hizi ambazo nimezitamka hapa. Engineering estimate zilikuwa dola za Kimarekani bilioni 3.006 sawa na shilingi trilioni 7.2, nasi tumesaini mkataba wa shilingi trilioni 5.2. Maana yake tumeokoa tena shilingi trilioni mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, kwa nini mkataba usivujwe? Huu makataba hatuwezi kuuvunja kwa sababu kwanza ni wa gharama nafuu; na pili, ni mkataba na CCECC. Ukiangalia rank za Makampuni yote duniani, perfomance ya kampuni hii, inaonesha kufanya vizuri, ni ya 10 kwa mwaka 2021, na ni ya 11 kwa mwaka 2022. Kwa hiyo, hata kipande kile cha kutoka Isaka - Mwanza ambacho ni kilomeeta 341, wana asilimia zaidi ya 30. Kwa hiyo, wanafanya vizuri na ndiyo maana tuliwapa mkataba huu wa kutoka Tabora kwenda Kigoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)