Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa sababu tatizo hili limekuwa kubwa karibu katika Wilaya zote nchini, kuna mlundikano wa kesi nyingi, lakini Wenyeviti hao wa Mabaraza ni wachache sana. Kwa nini Serikali isiwe na mkakati maalum kuhakikisha kwamba mabaraza yote ya ardhi katika Wilaya zetu yanapata Wenyeviti hawa? Swali la pili, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina mlundikano mkubwa wa kesi, ina migogoro mingi inayohusu ardhi: Je, Serikali haioni haja ya kupeleka Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi atakayekaa pale kwa ajili ya kuondoa migogoro na kutatua kesi zilizopo zinazohusu masuala ya ardhi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia jibu la msingi ambalo nimelitoa, ni kwamba sasa hivi tunaendelea na michakato kama nilivyoeleza, ya kuziba pengo la Wenyeviti 57 ambao utaratibu wake ukikamilika, tutakuwa tumekamilisha Wilaya zote hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Ukerewe, kutokana na mlundikano wa kesi, hili tutaliangalia kwa umuhimu wake na tutalifanyia kazi, ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mwaka 2018 Waziri wa Ardhi alitembelea mipaka ya Wilaya ya Monduli - Longido, Monduli - Arumeru, na Monduli - Babati na kuagiza mipaka hii iainishwe: Je, ni lini Serikali itaenda kutembelea mipaka hii na kuibainisha ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima kwa wananchi inayopelekea mapigano? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali la msingi lilihusu masuala ya Mabaraza. Kwenye eneo hili la mipaka, tayari tumeshaanza hiyo kazi na katika kipindi cha kama miezi miwili iliyopita, tulikuwa Mkoa wa Arusha ambapo tulitembelea ile mipaka inayotenganisha nchi na nchi. Kwa maana ya migogoro iliyopo kati ya wilaya na wilaya, tayari timu mbalimbali zimeshaundwa na zinakwenda kufanyia kazi haraka sana na Monduli na Arusha zitakuwa ni moja kati ya maeneo ya kupitiwa.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Wilaya ya Kahama ina Halmashauri tatu, lakini ina mwenyekiti mmoja tu wa Baraza la Ardhi. Sasa Serikali ina makakati gani wa kupeleka Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi katika Halmashauri ya Ushetu?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi kama nilivyolieleza katika jibu la msingi, tunaendelea na michakato ya kupata Wenyeviti katika kuziba pengo la karibu Wilaya 57, na tukishafanikisha, Ushetu nayo itapewa umuhimu wa pekee nao katika kufikishiwa Mwenyekiti wa Baraza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu, katika maeneo yote hapa nchini ambayo mabaraza hayajafika, Mamlaka za Miji husika, kama kuna majengo ambayo tayari yapo, ambayo tunaweza tukayatumia katika kipindi hiki, basi tuarifiane, na Waheshimiwa Wabunge kwenye maeneo yenu mtupe taarifa ili tuweze kuona uharaka wa kuwaleta wenyeviti wetu katika maeneo husika, ahsante sana.