Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza kujenga Mradi wa Maji katika Vijiji vya Sawala, Mtwango, Rufuna na Kibao vilivyopo Mufindi Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali, Mbunge wa Mufindi Kusini Mheshimiwa David Kihenzile, amekuwa akipigania sana na akiomba ukarabati wa mradi wa Imayi, yaani Kata za Ihoanza, Malangali na Idunda; na ule wa Vijiji tisa wa Kata za Mbalamaziwa na Itandula, lakini mpaka sasa haujaanza: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha? Pamoja na kwamba mmesema fedha zimetengwa, lini Serikali itapeleka fedha mradi huo uweze kufanikiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Mradi wa watumia maji wa Magubike, Kata ya Nzihi Jimbo la Kalenga umejengwa na wafadhili wa Marekani wanaoitwa WARIDI, lakini tayari walishajenga intake na tank lipo tayari, changamoto ni namna ya usambazaji wa maji kwenda katika vijiji sita pamoja na vitongoji vyake: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kupeleka miundombinu hiyo wananchi waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRTI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara tumejipanga vizuri, mradi huu wa Mbalamaziwa ambao unaenda kuhudumia vijiji tisa, tayari tumeshapata Mkandarasi na tunatarajia bajeti ijayo Mkandarasi huyu aanze kazi kwa sababu kila kitu kimeshakamilika. Mradi wa Malangali ni mradi mkubwa ambao tunatarajia utatumia zaidi ya Shilingi bilioni sita. Dhamira njema ya Mheshimiwa Rais ya kumtua Mama ndoo kichwani inaenda kukamilika kwa sababu bajeti ijayo tutahakikisha tunaleta fedha kwa awamu na kwa wakati ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, na wananchi waweze kunufaika na maji safi na salama ya kitoka bombani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la intake na tenki kukamilika kwenye Jimbo la Kalenga, tayari tunaendelea na utaratibu kuona kwamba usambazaji wa maji tunakuja kuufanya ndani ya bajeti hii tunayoimalizia, pia kwa bajeti ijayo, tutakuja kuhakikisha maeneo yote ambayo yanapaswa kufikiwa na maji, yanakwenda kufikiwa. (Makofi)

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza kujenga Mradi wa Maji katika Vijiji vya Sawala, Mtwango, Rufuna na Kibao vilivyopo Mufindi Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, tokea Tanzania imepata uhuru, kuna vijiji mkoani Mara hawajawahi kuyaona maji toka Setikalini: Je, Serikali ina mpango gani kupeleka maji katika Wilaya ya Serengeti na vijiji vyake na Wilaya nyingine ambazo zinazungukwa na utajiri wa Ziwa Victoria? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Marwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya aliyoyataja katika eneo la Serengeti, tayari tuna miradi ambayo tunatarajia wananchi waweze kunufaika na maji safi bombani. Nasi Wizara ya Maji, toka tumeanza kuhakikisha tunaleta mageuzi ndani ya Wizara hii, maeneo ambayo hayajawahi kupata maji, yanapata maji sasa hivi. Hivyo, wananchi wa Serengeti nao wakae mkao wa kupata maji safi na salama bombani.