Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Water and Irrigation Wizara ya Maji 285 2023-05-10

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza kujenga Mradi wa Maji katika Vijiji vya Sawala, Mtwango, Rufuna na Kibao vilivyopo Mufindi Kusini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika Kata ya Mtwango, na miradi imekamilika kwenye Vijiji vya Sawala na Mtwango. Kwa sasa miradi inaendelea katika Vijiji vya Rufuna na Kibao ambapo utekelezaji umefikia asilimia 52. Kazi zinazoendelea ni pamoja na ulazaji wa mabomba umbali wa Kilometa 21, ujenzi wa matenki mawili yenye jumla ya ujazo wa lita 450,000 na vituo 21 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa kazi hizo utakamilika mwezi Julai, 2023 na wananchi kupata huduma ya maji safi na salama.