Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia ujuzi na mafunzo?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, ni ukweli usiofichika kwamba SIDO zetu nyingi zinafanya kazi chini ya kiwango na hiyo ndiyo maana unaona hata idadi ya wanufaika ni wachache. Je, nini mpango wa Serikali wa kuziwezesha SIDO hizi ili ziweze kuwanufaisha wajasiriamali wengi zaidi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wajasiriamali wengi wanashindwa kumudu gharama za mafunzo haya. Je, Serikali iko tayari kuweka wazi na kutoa maelekezo kwa SIDO zote nchi nzima kutoa mafunzo haya bure na kuweka mwongozo wazi wa namna gani mafunzo haya yanafanyika katika SIDO zetu? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ni kweli, niungane na hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna changamoto ya bajeti kidogo kwa Shirika letu la SIDO lakini sasa ni mpango wa Serikali kuona baada ya kuongeza katika sekta nyingine, ni dhahiri tutakuja kwenye sekta hii ya viwanda ambapo SIDO ni wadau muhimu sana kuhakikisha wanaendeleza na kufanya kazi zao kwa weledi wakiwa na bajeti ya kutosha. Kwa hiyo, Serikali imejipanga kuongeza fedha ili waweze kuongezewa SIDO waweze kufanya kazi zao zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ni kweli tungeweza kutoa bure mafunzo lakini lazima kuna gharama ndogo ambazo wajasiriamali wanatakiwa kuchangia. Hoja kubwa hapa ni kuona namna gani tunawawezesha SIDO ili wawe na fedha za kutosha na gharama za wajasiriamali kuchangia kupata mafunzo ziwe chini zaidi au hatimaye yaweze kutolewa bure kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)