Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 284 2023-05-10

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia ujuzi na mafunzo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo nchini (SIDO), lenye ofisi katika Mikoa yote nchini hadi kufikia Februari 2023, imeratibu na kutoa mafunzo na ujuzi kwa wajasiriamali wapatao 12,091, ambapo wanaume walikuwa 5,082 sawa na asilimia 42 na wanawake 7,009 sawa na asilimia 58 kupitia kozi 519 katika maeneo mbalimbali yanayohusiana na uendelezaji wa biashara na shughuli za uzalishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kutoa mafunzo na ujuzi katika nyanja mbalimbali kwa wajasiriamali nchini. Aidha, Serikali imepanga kuongeza wigo wa kutoa mafunzo ya biashara na ufundi pamoja na ushauri kwa kutumia TEHAMA. Nakushukuru.(Makofi)