Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama yenye hadhi ya Wilaya katika Wilaya ya Kalambo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya Mahakama za Mwanzo katika Tarafa za Mwimbi, Kasanga na Mwazye na Mambwe Nkoswe ni chakavu kwelikweli. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wakati ikiwa inafikiria kujenga Mahakama mpya za Mwanzo?

Swali la pili; kwa kuwa Tarafa ya Mambwe Nkoswe ambayo ni kilometa 150 kwenda Makao Makuu ya Wilaya haina kabisa hata Mahakama ya Mwanzo. Je, Serikali iko tayari kwa uharaka kuhakikisha kwamba tunajengewa Mahakama ya Mwanzo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephat Kandege, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu wa fedha Mahakama imetenga fedha kwa ajili ya kujenga Mahakama katika Kata hii ya Kasanga ambayo ni hitaji la Mheshimiwa Mbunge. Kwa Tarafa ambayo ameitaja katika swali la pili, naomba nimuarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba Mahakama itaendelea kutenga fedha kukamilisha Mahakama za Mwanzo ambazo hazijajengwa katika maeneo ambayo kuna uhitaji, ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama yenye hadhi ya Wilaya katika Wilaya ya Kalambo?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mahakama ya Wilaya ya Kiteto ni ya zamani kidogo na majengo yamechakaa. Kwa jibu la uhakika kabisa, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya kwenye Jimbo la Kiteto?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Edward Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa Mahakama, Mahakama ya Wilaya ya Kiteto itajengwa katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama yenye hadhi ya Wilaya katika Wilaya ya Kalambo?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Serikali ilituahidi kujenga Mahakama ya Mwanzo Tarafa ya Namanyere, ninapenda kujua utaratibu huo umefikia wapi.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka ujao wa fedha wa 2023/2024 kwa bajeti yetu ambayo tumepitisha tunakwenda kujenga Mahakama katika Kata ya Namanyere na katika Wilaya ya Nkasi.