Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara nyingi za Jiji la Dar es Salaam, hasa zile zilizo chini ya TARURA huhitaji matengenezo ya mara kwa mara. Je, Serikali haioni ipo haja kwa TARURA kuwa na kitengo maalum cha matengenezo badala ya kuwatumia Wakandarasi?

Swali la pili, kwa kuwa Jimbo la Kinondoni linazungukwa na mito midogo midogo ambayo husababisha mafuriko hasa katika Kata za Mwanayamala, Kijitonyama, Tandale, Kigogo na Ndugumbi. Je, Serikali ipo tayari kufanya upembuzi wa kitaalam ili kubaini njia bora za kukabiliana na hali hii ya mafuriko?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la kwanza la Mheshimiwa Tarimba la je, TARURA ipo tayari kuanzisha kitengo maalum kwa ajili ya kuangalia ukarabati wa barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuanzisha kitengo maalum kunahitaji rasilimali fedha, rasilimali watu na vifaa. Hivyo basi, kwa sasa TARURA inaona ni bora kufanya outsourcing kwa sekta binafsi. Hii pia inasaidia kutoa ajira kwa Watanzania wengine ambao wanafanya kazi katika sekta binafsi. Vilevile ina-assure quality control na kunakuwa kuna checks and balances akipewa mtu na TARURA wakamkagua.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, tayari mito ya Jimbo la Kinondoni imetengewa fedha kwenye Mradi wa DMDP II ambao utaanza Novemba, mwaka huu 2023. Kwenye DMDP I tayari walikuwa wameshatengenezewa Mto Ng’ombe ambayo imezuia mafuriko makubwa sana katika maeneo yanayozunguka barabara hizi na makazi ya watu wa Jimbo la Kinondoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wakati Kinondoni wanaomba fedha kwa ajili ya kujengewa lami, Wilaya ya Makete na Mkoa wa Njombe tunaomba fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za changarawe kwenye barabara ya kutoka Kinyika – Kikondo – Nkenja – Ikuwo, barabara ambazo zimeharibika sana kutokana na mvua nyingi zinazoendelea Jimboni Makete.

Je, Serikali itafanya nini itusaidie tupate fedha hizo kwa sababu barabara hizi ni barabara za uzalishaji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mwaka wa fedha huu Bunge lako tukufu limeipitishia TARURA bajeti ya zaidi ya bilioni 772 tutaangalia barabara hii ya Kinyika – Kikondo katika Jimbo la Makete kule kama nayo imetengewa fedha kwenye bajeti hii. Kama haijatengewa fedha tutaangalia mwaka wa fedha unaofuata tuweze kutenga fedha kwenye bajeti kutengeneza barabara hii.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wananchi wa Wilaya ya Tanganyika wanapakana na Wilaya ya Nkasi Kusini na upande wa Kaskazini wanapakana na Wilaya ya Uvinza. Maeneo haya kwa wananchi wanaoishi mwambao wa Ziwa hawana njia mbadala tofauti na njia ya majini.

Je, ni lini Serikali wataongeza bajeti kwa upande wa TARURA ili tuzifungue hizi njia tuepushe maafa kwa wananchi na mali zao? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ni lengo la Serikali kuiongezea TARURA fedha. Kama mlivyo mashahidi, mwaka wa fedha 2021/2022 bajeti ya TARURA nchi nzima ilikuwa shilingi bilioni 228, lakini baada ya bajeti ya 2021/2022 chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, TARURA imeongezewa fedha zaidi ya mara tatu kwenda shilingi bilioni 772. Tutaangalia hizi barabara zinazounganisha Tanganyika, Nkasi na Uvinza ili ziweze kupata fedha na kutengenezwa, kadri ya fedha itakavyopatikana.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafsi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Barabara ya Banana – Kitunda – Kivule – Msongola inatajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ukurasa wa 78, kilometa 11.5, na mpaka sasa Serikali imetenga kilometa 2.2 tu. Ni lini Serikali sasa itatenga fedha za kumalizia kilometa 9.3 ili kutekeleza ahadi iliyoko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge ya Msongola ya kilometa 2.2 ambayo ndiyo imetengewa fedha, tayari nilikaa na Mheshimiwa Mbunge, alikuja kulifuatilia na lenyewe na tukakaa na wataalam wa TARURA kuhakikisha kwamba tunaona ni namna gani tunapata fedha hii ya kilometa 9.3 iliyosalia kama ambavyo iliahidiwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakaa kuangalia tunafanya vipi ili fedha hizi ziweze kupatikana na barabara hii iweze kutengenezwa.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya Suka – Golani ambayo ilianza kujengwa mwaka jana, kilometa nane zimeshajengwa mita 400 lakini imesimama baada ya flow ya fedha kushuka.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza akaahidi hapa kwamba mwaka huu flow ya fedha itakuwa nzuri kwa barabara hii ili wananchi wahakikishiwe kwamba barabara inakamilika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, baraba hii ya Suka – Golani kama ambavyo nimeshasema hapa kwenye baadhi ya maswali niliyoulizwa, kwamba TARURA imeongezewa fedha sasa na tutaangalia kupitia Meneja wa TARURA katika Mkoa wa Dar es Salaam na Wilaya ya Ubungo kuona ni namna gani katika bajeti ambayo ameitenga barabara hii itaweza kuendelea kufanyiwa matengenezo.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Katika Jimbo letu la Kilwa Kaskazini lina mtandao wa barabara za TARURA kilometa 528 ambazo zote ni za vumbi. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hizo kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA itaanza kujenga barabara za lami katika Jimbo la Kilwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ninarudia tena tayari TARURA imeongezewa bajeti na Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tutaangalia na Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Lindi na Wilaya ya Kilwa kuona katika bajeti ambayo imepitishwa hapa ni kilometa ngapi ya lami ambayo imetengwa ili katika hizi barabara za Kilwa alizotaja Mheshimiwa Ndulane angalau moja ianze kupata lami.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kigamboni ina mtandao wa barabara za TARURA takribani kilometa 1,000, lakini ni kilometa tano tu ambayo ni asilimia 0.5 percent ambazo zina kiwango cha lami. Bajeti ya TARURA pale ni shilingi bilioni 3.5.

Je, nini mkakati wa TARURA kuongeza bajeti ili barabara za Wilaya ya Kigamboni zifanane na barabara nyingine za Jiji la Dar es Salaam?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA itaendelea kuongeza fedha katika Wilaya ya Kigamboni na Jimbo la Kigamboni kwa Mheshimiwa Ndugulile kadri ya upatikanaji wa fedha. Ni lengo la Serikali hii ya Awamu ya Sita kuhakikisha TARURA inakuwa na nguvu ya kutosha kutengeneza barabara nyingi zaidi za lami katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo kule Kigamboni.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Akheri inayoanzia Sangisi kwenda Ndoombo ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne kujengwa kwa kiwango cha lami miaka kumi iliyopita. Mwaka jana barabara hiyo imeanza kujengwa: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuimalizia mwaka huu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Akheri – Sangisi ambayo ameitaja Mheshimiwa Dkt. Pallangyo hapa ambayo tayari imeshaanza kuwekewa lami itaendelea kuwekewa lami kwa sababu ni ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kadri ya upatikanaji wa fedha na tutaendelea kuitengea bajeti kwenye miaka ya fedha ambayo inafuata.