Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 282 2023-05-10

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaongezea TARURA bajeti ili barabara za ndani ya Jimbo la Kinondoni zijengwe kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikiongeza bajeti kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022, Jimbo la Kinondoni lilitengewa bajeti ya shilingi bilioni 2.38 ambazo zilitekeleza matengenezo ya barabara ya jumla kilometa 26 za lami na changarawe na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ya kilometa 0.52. Hii ni sawa na ongezeko la asilimia 32 ya bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 ambapo bajeti ilikuwa ni shilingi bilioni 1.8.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Jimbo la Kinondoni lilitengewa bajeti ya shilingi bilioni 4.87 kwa ajili ya kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara zenye jumla ya kilomita 26.52, ambapo matengenezo ya kawaida ni kilomita 24.32 na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kilometa 2.2 ambapo utekelezaji wake unaendelea na umefikia asilimia 70. Hii ni sawa na ongezeko la asilimia 29 ya bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuiongezea fedha TARURA kwa ajili ya kuongeza mtandao wa barabara za lami katika Jimbo la Kinondoni na maeneo mengine kwa kadri ya upatikani wa fedha.