Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani kuondoa tatizo la wanafunzi kusoma kwa zamu katika Halmashauri ya Mji Tarime?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna shule katika Mji wetu wa Tarime inaitwa Bugosi, ina zaidi ya wanafunzi 1,000 lakini ina madarasa Sita na wananchi wamejitahidi sana kujenga lakini jitihada za Serikali kuwatia nguvu inakuwa ni kidogo: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga madarasa ya kutosha katika shule hii? (Makofi)

Swali langu la pili, zipo jitihada za wananchi wanazofanya kuhakikisha kwamba wanajenga shule mpya. Kwa mfano katika Kata ya Kenyamanyori kuna Shule zinaitwa Chira, Nyamitembe na shule nyingine ambazo zimejengwa na zimefika katika hatua ya upauaji lakini Serikali haijapeleka fedha kwa ajili ya kumalizia na shule zile zifunguliwe: -

Je, ni lini fedha zitapelekwa ili majengo yale yakamilike na wanafunzi waweze kusoma? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kembaki.

Swali lake la kwanza kwenye hule hii ya Bugosi yenye wanafunzi zaidi ya 1,000 na madarasa Sita, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba tunapeleka shilingi bilioni 1.5 katika Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa shule hizi kupunguza msongamano. Kwa hiyo Serikali iko tayari kupeleka fedha na tayari imeshatengewa.

Swali lake la pili, kwenye Kata hii ya Kenyamanyori, nitaa na Mheshimiwa Kembaki tuweze kuangalia upungufu ambao upo katika shule hizi alizozitaja za vijiji vya Kata hii, ili tuone ni namna gani tunaweza tukafanya kuweza kukarabati shule hizi ama kuongeza madarasa.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani kuondoa tatizo la wanafunzi kusoma kwa zamu katika Halmashauri ya Mji Tarime?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shule ya Msingi Kizota ambayo iko katika Jiji la Dodoma ni miongoni mwa shule ambazo zina wanafunzi wengi sana na hivyo kusababisha wanafunzi kuingia kwa zamu.

Nini mkakati wa Serikali wa kujenga shule katika eneo la mnada mpya ambapo hakuna shule kabisa kwa sababu watoto wengi wanatokea eneo lile?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari kujenga shule nyingi kwa wakazi wa kule Kizota kadri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika mradi huu wa BOOST ambao Waheshimiwa Wabunge ninyi ni mashuhuda, fedha nyingi sana imetolewa na Serikali hii ya awamu ya Sita kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa shule tuone ni namna gani tunaweza tukafanya kwa ajili ya wakazi wa Kizota wapate shule nyingine na wanafunzi waache kwenda kwa zamu pale.