Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 281 2023-05-10

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani kuondoa tatizo la wanafunzi kusoma kwa zamu katika Halmashauri ya Mji Tarime?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Mwita Kembaki, Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime imeshatenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ili kuondoa msongamano wa wanafunzi pamoja na kuondoa tatizo la wanafunzi kusoma kwa zamu. Baadhi ya maeneo tayari wananchi wameanza kujenga shule, mfano Kata ya Turwa, Chirya, Kenyamanyori.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na jitihada hizo za wananchi, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya, hii itasaidia kuongeza madarasa katika shule za msingi na hivyo kuondokana na msangamano wa wanafunzi darasani.