Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kutoka Kigwe B hadi Magiri Uyui ili kuchepusha magari makubwa kupita Tabora Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, majibu yaliyotolewa na Serikali yamejielekeza kwenye barabara ndogo iliyokuwepo wakati swali langu lilikuwa ni kutaka barabara kubwa ili malori yasipite mjin,i (barabara ya pete), kwa hiyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, Serikali iko tayari kujenga barabara ya pete kutoka Kigwa B kwenda Magiri ili kuepusha magari makubwa yanayokwenda Burundi na Rwanda kupita Mjini na kuharibu barabara za Mjini?

Swali la pili, kwa vile Miji yote inayojengwa sasa ina barabara za pete pamoja na Jiji letu la Dodoma na Mji mdogo wa Nzega. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara za pete kuzunguka Mji wa Tabora?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kadiri ya upatikanaji wa fedha, lakini tayari katika bajeti hii ya 2023/2024 TARURA imetenga fedha ya kufanya upembuzi yakinifu kujua gharama jumla itakuwa ni kiasi gani kwa ajili ya ujenzi wa lami wa barabara hii. Hivi ilivyo sasa bado ina uwezo wa kubeba malori na ndiyo maana tunaifanyia periodic maintenance.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu barabara za pete (ring roads); Serikali iko tayari kujenga barabara ya pete (ring road) katika Mji wa Tabora, tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi kuweza kuona tunaanzaje mchakato wa kufanya feasibility study ili Mji huu wa Tabora uweze kupata barabara hiyo ya pete.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.