Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 280 2023-05-10

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kutoka Kigwe B hadi Magiri Uyui ili kuchepusha magari makubwa kupita Tabora Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara ya mkato kutoka Kigwa B mpaka Magiri - Uyui Serikali imekuwa ikifanya matengenezo ya mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa barabara hiyo inapitika wakati wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali itatenga shilingi milioni 125 kwa ajili ya kufanya matengenezo ya muda maalum ya kilomita Saba kwa kuziwekea changarawe na kujenga kalavati moja ili iweze kuendelea kupitika muda wote na kutoa huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kuifanyia matengenezo na kujengwa kwa kiwango cha lami kadri ya upatikanaji wa fedha.