Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Gari la Zimamoto katika Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Songwe una halmashauri tano na magari yako katika halmashauri mbili ambayo ni halmashauri ya Wilaya ya Mbozi na Halmashauri ya Mji wa Tunduma, lakini kuna halmashauri ya Ileje, Momba na Songwe mpaka sasa hayana magari ya zimamoto.

Je, mnatumia njia gani kukabiliana na majanga ya moto yanapotokea katika Wilaya hizi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa magari yaliyopo katika Wilaya ya Halmashauri ya Mbozi na Halmashauri ya Mji wa Tunduma ni magari madogo hayana uwezo mkubwa wa kukabiliana na majanga makubwa ya moto.

Je, ni lini mpango wa Serikali kuhakikisha wanaleta magari makubwa na ya kisasa kwa akili ya kukabiliana na majanga ya moto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, ni kweli tunatambua uwepo wa Halmashauri tatu za Wilaya ambazo hazina magari, na ndiyo maana kwenye jibu la msingi nimesema tunaendelea kuliwezesha Jeshi la Zimamoto hatua kwa hatua kutegemea upatikanaji wa fedha. Hata hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wabunge wa majimbo, akiweno Mwenisongole amewasiliana na Wizara kwa kaaribu na Mkuu wa Fire nchini na tumewaahidi kuwapa gari moja hata kabla ya magari ambayo tuna plan kununua hatujanunua.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu uwezo mdogo wa magari tunatambua, ndiyo maana kwenye bajeti ijayo ambayo tutaleta tuombe Bunge lako lituhidhinishie ipo bajeti ya kununua magari makubwa na kadri yatakavyokuwa yananunuliwa tutakuwa tunapeleka kwenye Wilaya zenye changamoto zikiwemo hizo Wilaya za Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Spika, niwashukuru watu wa Songwe, kwenye wilaya tatu alizozitaja hakuna matukio ya mara kwa mara ya majanga ya moto yanayohitaji uokoaji. Tunashukuru kwamba elimu ya zimamoto na wokozi wanaizingatia wananchi wa Mkoa huo. Ahsante.