Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 246 2023-05-05

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Gari la Zimamoto katika Mkoa wa Songwe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Songwe lina magari mawili ya kuzima moto. Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe Wilaya ya Mbozi Mji Mdogo wa Vwawa kuna gari moja aina ya Fuso yenye namba za usajili ZT 0014. Gari hilo linaujazo wa lita 1,500 za maji na lita 500 za foam. Katika Wilaya ya Tunduma kuna gari moja aina ya Mitsubish Canter yenye namba za usajili STL 4914 na lina ujazo wa lita 1,200 za maji.

Mheshimiwa Spika, Aidha, Serikali itaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kuliongezea wataalam na vitendea kazi ikiwemo magari ya kuzima moto na uokoaji kwa Mkoa wa Songwe kwa madhumuni ya kuzifikia wilaya zote kutegemeana na upatikanaji wa fedha.