Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kufufua jengo la viwanda vidogo vidogo – Lwosaa?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nataka nimhakikishie Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba eneo hili limepimwa na lina hati ya Kijiji kwa ajili ya shughuli hiyo, na tayari Katibu Mkuu alitembelea eneo hili kwa hiyo hakuna mgogoro wowote wa umiliki.

Swali langu, kwa kuwa ujenzi huu umesimama tangia mwaka 1974 na sasa ni miaka 47 haujaendelezwa; je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi?

Swali la pili, kwa kuwa kuna kiwanda cha aina hiyo hiyo kimejengwa kata ya Rundugai na kimefadhiliwa na mradi wa TASAF; je, hatuoni iko haja ya Serikali kuchukua na kukiweka chini ya SIDO ili kiweze kutoa huduma?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; kwanza niwapongeze sana wananchi wa Jimbo la Hai kupitia Mbunge mahiri, ndugu yangu Saashisha Mafuwe kwa ufuatiliaji lakini pili kwa kutenga haya maeneo mahsusi na kuanza ujenzi wa jengo hilo ambalo ni muhimu sana kwa ajili ya maendeleo ya Viwanda.

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie wana- Hai na hasa wana- Lwosaa kwamba sisi kama Wizara tutahakikisha tunaendeleza jitihada hizi za wananchi katika kujiwekea maendeleo kupitia SIDO na taasisi zetu nyingine kuanza kukamilisha jengo hilo. Kama umiliki sasa ukihamishiwa kwenda SIDO maana yake tutakuwa na ule uhakika wa kuendeleza na kuwekeza zaidi katika ujenzi wa jengo hilo na kukamilisha kama ambavyo tumesema kwa sababu tathmini imeshakamilika.

Mheshimiwa Spika, lakini pili na hili jengo lingine ambalo katika kata hiyo mpya Mheshimiwa Mbunge amesema nalo sasa wakati wanakuja kufanya uhamisho wa umiliki wa eneo hili la Lwosaa nawaagiza SIDO watembelee na kukagua pia jengo hili ili nalo tuweze kuliwekea katika mipango la kuliendeleza na kuwajengea wananchi hawa chuo cha ufundi kupitia SIDO katika Jimbo la Hai.

Mheshimiwa Spika, pia nichukue nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wengine wote na sisi wananchi tutenge maeneo kwa ajili ya maendeleo ya viwanda pamoja na masoko kwa ajili ya kujiletea maendeleo kupitia SIDO na taasisi nyingine.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.