Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 245 2023-05-05

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kufufua jengo la viwanda vidogo vidogo – Lwosaa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha tathmini ya jengo hilo na kupata gharama za ukarabati wa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo ambazo ni jumla ya shilingi 293,986,850. Pia Serikali kupitia SIDO inaendelea kufuatilia suala la umiliki wa eneo hilo ili kuanza ukarabati na kumalizia ujenzi. Aidha, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati na kukamilisha ujenzi wa jengo hilo ili shughuli kusudiwa zianze kufanyika kwa manufaa ya wananchi wa Lwosaa na Taifa kwa ujumla. Nakushukuru.