Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, kwa mujibu wa master plan ya miundombinu ya barabara Tanzania, tunahitaji fedha kiasi gani kukamilisha miundombinu hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Spika,ahsante sana, na nimpongeze Waziri kwa niaba ya Serikali kwa majibu mazuri sana, ila nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, hizi kilometa 25172.42 zilizo bakia ambazo zimejengwa kwa changarawe zitajengwa lini kwa lami na zitatumia muda gani?

Swali la pili bajeti hii ya bilioni 1.8 ninavyoamini ni pamoja na kujenga michirizi au mifereji ya maji sasa kuna maeneo ambayo mifereji hii haijajengwa hata hapa Mjini Dodoma; je, ni lini mifereji hii itajengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo : -

Mheshimiwa Spika,kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, fedha inayokadiriwa kukamilisha mtandao wa barabara ambazo zinahudumiwa na TANROADS ni takribani tirioni 45; na bado barabara zingine zinaendelea kupandishwa daraja kuja, kwa hiyo zitaendelea kuongezeka.

Mheshimiwa Spika,na Serikali kusema ni lini tunaweza tukakamilisha ujenzi wa barabara zote kwa kiwango cha lami hii itaendelea kuwa ni kazi endelevu kadri fedha inavyopatikana. Kwa sababu, Mbunge atakubaliana nami kwamba bajeti tu ya nchi kwa mwaka ni zaidi ya tirioni 40 kwenda 41 kwa bajeti tunayoitekeleza sasa barabara hizi ni tirioni 45 kwa hiyo Serikali inajitahidi kujenga barabara kadri ya uwezo lakini hasa barabara zile za kipaumbele. Kwa hiyo kadri tutakavyoendelea tunahakikisha tutaendelea kupunguza idadi ya barabara za changarawe.

Mheshimiwa Spika,kuhusu swali lake la pili, ni kweli barabara zinajengwa lakini zingine hazina mitaro, lakini kipaumbele za kuweka mitaro hasa ni barabara ambazo ziko kwenye miji na maeneo ambayo wananchi wako wengi kwa ajili ya usalama. Na changamoto kubwa ambayo tunaipata kwenye uzibaji wa mitaro ni pale ambapo huduma za kijamii zinasababisha ile mitaro inaziba na basi maji hayo yanapanda kwenye barabara na kuharibu zile barabara.