Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 244 2023-05-05

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, kwa mujibu wa master plan ya miundombinu ya barabara Tanzania, tunahitaji fedha kiasi gani kukamilisha miundombinu hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inasimamia mtandao wa barabara wenye urefu kilometa 36,760.29, kati hizo kilometa 12,223.04 ni barabara kuu (Trunk Roads) na kilometa 24,537.25 ni barabara za mkoa (Regional Roads). Kati ya kilometa 36,760.29, kilometa 11,587.82 sawa na asilimia 31.50 zimejengwa kwa kiwango cha lami na kilometa 25,172.48 zilizobaki ni za changarawe, sawa na asilimia
68.50. Ili kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 25,172.48 zilizobaki, inakadiriwa kiasi cha shilingi trilioni 45.3 zinahitajika kwa wastani wa gharama za ujenzi bilioni 1.8 kwa kilometa kilometa moja, ahsante.