Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga meli katika Bandari ya Mtwara itakayorahisisha mawasiliano na nchi ya Comoro?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, suala la upembuzi yakinifu limechukua muda mrefu sana, ndiyo kwanza saa hizi Serikali imejipanga kuanza kutenga fedha.

Je, Serikali haioni kwamba ujenzi wa bandari katika mwambao wa Bahari ya Hindi ungerahisisha sana na kupunguza suala la ukosefu wa ajira kwa wananchi wa Tanzania, hususan wa Mikoa ya Kusini ya Mtwara na Lindi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mkoa wa Mtwara unalima mazao ya mihogo, njugu, mbaazi, nazi, mazao ambayo yanahitajika sana kule Comoro. Je, Serikali haioni kwamba kama kungekuwa na meli hii uwepo wake ungechechemua sana uchumi wa watu wa Mikoa ya Mtwara, Lindi pamoja na Ruvuma? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imechukua muda mrefu kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na ulianza tangu mwaka 2019 na 2021. Hii ilikuwa ni kwanza lazima ilitakiwa tujiridhishe – na huu ulikuwa upembuzi yakinifu wa awali – tujiridhishe kiasi cha mzigo utakaotoka Mtwara kwenda Comoro ili tujue ni aina gani ya mali na ukubwa wake, ambaye Serikali kwayo itakwenda kujenga ama kutengeneza.

Mheshimiwa Spika, lakini hata hivyo, kwa kuwa katika Mwaka wa Fedha ujao tumetenga fedha sasa kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa kina wa mwisho ili tupate uhalisia wa aina gani ya meli hii.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili; Serikali inatambua juhudi za wakulima wa Mtwara, hususan wale wote ambao wanalima mazao mbalimbali. Na kuna kila sababu ya kwamba wawe na meli inayosafirisha mazao yao kutoka Mtwara kwenda Visiwa vya Comoro.

Mheshimiwa Spika, na kwa jitihada hizo, kupitia Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ziara aliyoifanya Ufaransa, ndiyo maana meli hizi sasa zimeshaanza kuja nchini, hususan katika Kampuni ya CMA, CGM pamoja na UFL Express, maana kwamba Mtwara itakuwa hub, na Nchi jirani kama Comoro, Mozambique pamoja na Malawi watakuwa wanachukua mizigo pale kwenda maeneo yao, ahsante.