Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 243 2023-05-05

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga meli katika Bandari ya Mtwara itakayorahisisha mawasiliano na nchi ya Comoro?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa mawasiliano baina yake na mataifa jirani, hasa Nchi ya Comoro. Serikali kupitia Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), imetenga fedha kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu (feasibility study) katika Bahari ya Hindi kwa lengo la kujiridhisha na kiwango cha mahitaji ya usafiri huo kwa wananchi wa mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi na nchi jirani ikiwa ni pamoja na Visiwa vya Comoro. Upembuzi huo utasaidia Serikali kuamua aina ya meli itakayojengwa kulingana na hitaji la wananchi na soko kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hatua hiyo ya kufanya upembuzi yakinifu, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari imefanikiwa kuishawishi Kampuni ya Meli ya CMA CGM kutumia Bandari ya Mtwara kama kitovu (hub) cha mizigo inayokwenda Visiwa vya Comoro. Hivyo, mizigo inayotoka Nchi za Ulaya na Asia kwenda Comoro na ile inayotoka Tanzania kwenda Comoro (transshipment) imeanza kuhudumiwa katika Bandari ya Mtwara.

Mheshimiwa Spika, meli ya Kampuni ya CMA CGM ilianza safari za kupitia Bandari ya Mtwara tarehe 20 Aprili, 2023 na itaendelea kutoa huduma hiyo kila baada ya wiki moja. Aidha, meli ya kwanza kutoka Mtwara kwenda Comoro iliondoka tarehe 02 Mei, 2023 na itaendelea kutoa huduma hiyo kila baada ya wiki mbili, ahsante.