Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. MWANAHAMIS KASSIM SAID aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo la watuhumiwa kutopewa dhamana kwa makosa yenye dhamana?

Supplementary Question 1

MHE. MWANAHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Spika, majibu anayoyajibu Mheshimiwa Waziri, mimi sina, sijayaona kwenye swali langu. Hapa sikuuliza sheria kwa sababu sheria haina matatizo, wale watekelezaji wa sheria ndio wenye matatizo.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, pamoja na jibu la msingi ambalo ni zuri kama alivyolieleza Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mbunge wa Magomeni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wasimamizi wa sheria ni pamoja na Jeshi la Polisi, na huenda dhamana anazozikusudia ni zile ambazo zinatolewa na Jeshi la Polisi lakini watu hawatoki. Jambo la msingi ambalo tumelifanya Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia IGP ni kuwataka RPCs, OCDs na wale wakuu wa vituo (OCSs), kukagua mara kwa mara mahabusu zetu na kuona watu waliomo ndani na sababu gani zimesababisha awe ndani ili waweze kuachiwa kama hakuna sababu za msingi.

Mheshimiwa Spika, lakini tumebaini pia kwamba kuna baadhi ya watu wanawekwa ndani hata ndugu zao wanagoma kuwawekea dhamana, na hii ni kwa sababu ya matukio ya mara kwa mara yanayojirudia kiasi kwamba yanafedhehesha jamii. Kwa hiyo, niwaombe pia ndugu wawe wepese kuwadhamini kwa wale ambao dhamana zinakuwa wazi.

Mheshimiwa Spika, tumewasisitiza wakuu wa vituo pale inapowezekana kwa makosa yanayodhaminiwa waweze kutoa dhamana. Na kama Mheshimiwa Mbunge ana jambo specific, niko tayari kukutana naye baada ya kipindi cha maswali na majibu ili tuweze kuambiwa halafu tuone ni kitu gani kilichokwama, nashukuru. (Makofi)