Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 242 2023-05-05

Name

Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. MWANAHAMIS KASSIM SAID aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo la watuhumiwa kutopewa dhamana kwa makosa yenye dhamana?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mbunge wa Magomeni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dhamana katika kesi za jinai ni haki ambayo imewekewa utaratibu wa kisheria. Kwa mujibu wa sheria zetu yapo makosa yanayodhaminika na yapo makosa ambayo hayana dhamana. Kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai Sura 20 kimeainisha makosa yote ambayo hayana dhamana. Hivyo, kwa makosa yote ambayo hayajatajwa na kifungo hicho yana dhamana ambayo ni haki ya mshtakiwa.