Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, lini Serikali itatekeleza mradi wa kusambaza maji kutoka Mlandizi hadi Mzenga – Kisarawe?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza niishukuru Serikali kupitia Mheshimiwa Waziri hapo, nimefuatilia leo na kupata uhakika kwamba mafundi sanifu wako site kwa ajili ya mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Tarafa hii ya Mzenga, na hususan Kata hii ya Mzenga, zikiwemo Kata za Vihingo, Kurui na Mafizi, zina shida kubwa ya maji, licha ya kwamba Serikali mmetoa commitment.

Je, ni namna gani Serikali inaweza kutusaidia kwa dharura ikizingatia tumeshapata lile gari la kuchimba visima? Na tunaishukuru sana Serikali.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali yetu ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya miradi mingi ya maji Mkoa wetu wa Pwani na Tanzania kwa ujumla.

Je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kuweza kupunguza gharama za kuunganisha maji, hasa vijijini, ili wanawake watumie maji majumbani ili iweze kuleta tija ya miradi mikubwa iliyofanyika? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowapigania wananchi katika Mkoa wa Pwani. Kubwa ambalo nataka nisisitize ni kwamba Mheshimiwa Rais ametupatia fedha juu ya ununuzi wa mitambo na mitambo tumekwisha inunua, niwaelekeze watu wa DDCA wafike katika haya maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyaomba ili tuweze kufanya tafiti za haraka na kuhakikisha visima hivi vinachimbwa wananchi hawa waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, amezungumza juu ya gharama za maunganisho, hasa kwa wananchi kupata maji majumbani. Tumekwishatoa maelekezo katika Wizara ya Maji na watendaji wanalifanyia kazi. Tunataka tuwe na bei elekezi, hasa juu ya maunganisho ya maji majumbani. Kwa hiyo tunalifanyia kazi na tumelipokea kuhakikisha kwamba gharama zake zinakuwa reasonable na wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.