Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 241 2023-05-05

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -

Je, lini Serikali itatekeleza mradi wa kusambaza maji kutoka Mlandizi hadi Mzenga – Kisarawe?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na usanifu wa kina wa mradi wa maji kutoka bomba kuu la DAWASA Mlandizi kupeleka kwenye vijiji 19 vya Wilaya ya Kisarawe vikiwemo vijiji vya Kata ya Mzenga. Usanifu huo unatarajia kukamilika mwezi Agosti, 2023 na ujenzi kufanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.